Walengwa wa Ujumbe katika Bembelezi za Watikuu

No Thumbnail Available

Date

2022-08

Journal Title

Journal ISSN

Volume Title

Publisher

East African Journal of Swahili Studies

Abstract

Nyimbo zikiwa za watoto, inatarajiwa kuwa walengwa watakuwa watoto wenyewe kwa kuwa maudhui yaliyomo yatawalenga. Bembelezi zilizotafitiwa katika tamaduni mbalimbali ulimwenguni zinaonyesha kuwa ujumbe uliyomo huwalenga watoto na wakati mwingine, mama na baba zao. Kimsingi, wanawake, kando na kuzitumia katika shughuli za kubembeleza watoto, huzitumia pia kama jukwaa la kujieleza na kutakasa mioyo yao kutokana na uchungu, mtamauko na mfadhaiko wa mawazo uliosababishwa na matatizo ya kindoa kutokana na mifumo ya kibabedume inayoendelezwa katika baadhi ya jamii. Makala hii inachunguza diskosi zinazojitokeza katika bembelezi za Watikuu ili kubaini walengwa wa ujumbe uliomo. Lugha inayotumiwa na wanawake katika uimbaji wa bembelezi hizi inatilia shaka iwapo ujumbe uliomo unalenga tu watoto au mna watu wengine wanaolengwa kando na watoto

Description

Journal Article

Keywords

Bembelezi, Walengwa, Washiriki, Ujumbe, Watikuu

Citation

Akaka, L., & Simwa, S. W. (2022). Walengwa wa Ujumbe katika Bembelezi za Watikuu. East African Journal of Swahili Studies, 5(1), 288-296. https://doi.org/10.37284/jammk.5.1.817.

Collections